Klabu ya Chelsea imeingia kwenye anga za kumuwania mshambuliaji wa Reims, Hugo Ekitike katika majira yajayo ya kiangazi kulingana na taarifa mbalimbali za michezo nchini ufaransa.

Ekitike, 19 anayekipiga katika klabu ya Reims nchini ufaransa amefanikiwa kufunga magoli 10 na kutoa pasi za magoli tatu katika mechi 23 alizocheza msimu huu.
Chelsea wanamuwania kinda huyo anayetarajiwa kufwata njia ya Didier Drogba, Michy Batshuayi na Eden Hazard ambao wote walipita katika klabu hiyo kabla ya kutua Stamford Bridge.
Kulingana na Jarida la Bild, Borrussia Dortmund, Newcastle United na West Ham ni moja ya vilabu vilivyoonyesha nia ya kupata huduma za mshambuliaji huyo wa ufaransa katika kikosi cha vijana wa chini ya miaka 20.
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


