Chiesa Awaweka Vitani Chelsea, City na Bayern.

Kulingana na Jarida la Calcio Mercato, Manchester City wamejiunga na mbio za kumsajili winga wa Juventus, Federico Chiesa.

Chelsea na Bayern Munich pia wamekuwa wakimfwatilia mchezaji huyo wa miaka 23, ambaye alikuwa na jukumu muhimu katika mbio za Italia za kutwaa taji la Euro 2020 mapema msimu huu wa joto.

Mchezaji huyo aliisaidia Azzurri kutwaa taji la Euro 2020 ambapo alifanikiwa kufunga magoli mawili katika mechi saba alizocheza katika mashindano hayo.

Chiesa amebakiza mwaka mmoja tu kwenye mkataba wake wa mkopo huko Juve, lakini imeripotiwa kuwa hawataki kumuuza msimu huu wa joto na wanataka kumnunua kwa mkataba wa kudumu kutoka Fiorentina.

Bado inaangaziwa kama Manchester City wataweza kumshawishi mchezaji huyo na klabu ya Juventus, baada ya dau la Chelsea la €100million (£86.3m) kukataliwa wiki iliyopita.


FURAHIA KASINO MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Kasino ya Mayan Eagle inakukufanya kuwa bingwa wakati wowote unapoamua kuicheza. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.