Mabingwa wa EFL waliopanda Ligi kuu EPL, Leeds United, wameshindwa kupata huduma ya kiungo wa Bayern Munich, Michael Cuisance, baada ya kufeli vipimo vya afya.
Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 21 amewahi kuchezea kikosi cha makinda wa Ufaransa. Alihamia Bayern mnamo Agosti 2019 baada ya kuagana na Borussia Monchengladbach ya Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga).
Cuisance aliwatumikia Bayern ambao ni wafalme wa Bundesliga na Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) katika msimu wa 2019-20 na kuwafungia bao moja. Taarifa za ndani zinasema makubaliano kati ya vilabu viwili yalikuwa magumu pia.
Mchezaji huyo alitokea benchi katika kipindi cha pili katika ushindi wa 8-0 walioupata Bayern dhidi ya Schalke 04 katika mechi ya kwanza ya Bundesliga msimu huu.
Cuisance alikuwa mchezaji wa akiba ambaye hakutumiwa katika mchezo wa Uefa Super Cup lililowakutanisha Bayern na Sevilla mnamo Septemba 24, 2020.
Hata hivyo, aliachwa nje ya kikosi kilichotegemewa na kocha Hansi Flick katika mechi ya Bundesliga iliyoshuhudia Bayern wakichezea kichapo cha 4-1 kutoka kwa Hoffenheim mnamo Septemba 27, 2020.
Cuisance alisalia benchi katika fainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) iliyoshuhudia Bayern wakizamisha chombo cha Paris Saint-Germain (PSG) kwa bao 1-0 jijini Lisbon, Ureno mnamo Agosti 23, 2020.
Leeds United ya kocha Marcelo Bielsa imesajili wachezaji wanne hadi kufikia sasa. Kikosi hicho kimewasajili Rodrigo Moreno kutoka Valencia, Diego Llorente kutoka Real Sociedad, Robin Koch kutoka Freiburg na aliyekuwa mshambuliaji wa zamani wa Wolves, Helder Costa.
Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!
Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!
Ester mmakasa
Daah! Tumemkosa kiungo imara .
Ernest
Kanani tena Cuisance juu ya afya yake adi kufeli vipimo vya Afya?
magdalena
duh leeds wamekocha mchezaji mahili sana
Sauda
Afya ndo kila kitu katika maisha.
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri kuhijua afya yako inapendeza nafya ndio kila kitu
Zeiyana
Leeds united wamekosa bonge la kiungo
Caroline
Mhh kuna nn tenaaa
Elika
Dah pole kwa Leeds..huyo kiungo angewafaa sana
Dorophina
Leeds wamemkosa mchezaji mzuri sana
Mwanahamisi
Pole yake leeds
Mwajumah
Leeds wamekosa bonge la mchezaji
Adelta
Pole Sana leeds
Venerose
Asante kwa taarifa
Nasra
Wakosa mchezaji wa maana sana leeds
Tatu
Leeds wanatakiwa kutafuta mtu mwingine
Janeflora malisa
Pole
Khadija
Asante kwa taarifa
Fatina mfingi
Pole yako
Hopemwaikuka
So sad
aisha
Pole sana cuisance kwa kukosa vipimo vya afya
Neema
Afya ndio mpango mzima
Zuhura omary kindamba
Hii si habali njema kabisa
Povel
Afya ni Bora mengne watapatikana tu
Saupha mohamed
Pole kijana
Shani
Leeds wangepata huduma ya huyu mtu ingekua ni safi
lombo
sad news
Issa
Mtu makin sana leeds wamekosa mtu
Sabrina
Duh sio poa
Angelina
Sio poa
Amiri Kayera
Dah deal limeota mbawa
Latifa juma mohamed
Daah! Tumemkosa kiungo imara .
Gabriel
huyo kiungo angewafaa sana Leeds
David Pere
Ametisha sanaa
Samiah
Safi