Licha ya kumpatia mkataba mnono wa miaka 8 wenye mshahara mkubwa, bado Declan Rice ameendelea kuwakataa West Ham United. Kazi iendelee.
Rice amebakiza miaka 2 (The Hammers wanachaguo la kuongeza mwaka 1 zaidi) kwenye mkataba wake na klabu hiyo na, kwa muda sasa amekuwa akizikataa ofa za kuongeza mkataba na klabu hiyo.
Kukataa mkataba mpya kwa Declan Rice kunazua maswali mengi kuelekea dirisha kubwa la usajili mwezi ujao ambapo, Chelsea na Manchester United zinahusishwa kuwania saini ya kiungo huyu.
West Ham United wamekuwa wakisisitiza kutomuuza Rice kwa gharama ya chini ya £100M ikiaminikiwa kuwa, huu ni mpango wa kutaka kuendelea kuviweka mbali vilabu vinavyomuwinda Declan Rice japokuwa hata yeye anaonesha nia ya kutaka kuondoka.
Nani atamfunga paka kengele? Ni Rice au West Ham atakayeshinda mbio hizi za vuta ni kuvute?
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.