Gasperini: "Sijavunjika Moyo Baada ya Roma Kuaga Coppa Italia"

Gian Piero Gasperini amesisitiza kuwa hajavunjika moyo baada ya Roma kutolewa kwenye Coppa Italia na Torino Jumanne usiku, akisema kuwa kipa Mile Svilar hana lawama kwa mabao yaliyofungwa, huku akimuelezea kijana wa miaka 16 Antonio Arena kuwa amekomaa sana kulingana na umri wake.

Gasperini: "Sijavunjika Moyo Baada ya Roma Kuaga Coppa Italia"

Roma iliondolewa Coppa Italia baada ya kufungwa 3-2 nyumbani na Torino. Mabao mawili ya Che Adams na bao la ushindi la dakika za mwisho kutoka kwa Emirhan Ilkhan yaliizamisha Roma, licha ya mabao ya Mario Hermoso na Arena aliyefunga kwa mguso wake wa kwanza katika soka la wakubwa.

Akizungumza baada ya mechi, Gasperini alisema ni vigumu kuongeza washambuliaji mwezi Januari, lakini akawasifu wachezaji wake kwa kiwango walichoonyesha. Alikiri kuna masikitiko juu ya mabao waliyofungwa, lakini akasisitiza kuwa hakuna mtu wa kulaumiwa. Kuhusu Arena, alisema bao lake ni ishara nzuri, akibainisha kuwa ana nguvu za mwili, ujasiri na stamina nzuri, na kwa umri wake ameendelea vyema sana.

Gasperini alihitimisha kwa kusema ameridhika na kiwango cha timu yake, akaomba radhi kwa mashabiki na kuonya kuwa ni changamoto kubwa kucheza mashindano yote, akisisitiza tena: “Sijavunjika moyo.”

Gasperini: "Sijavunjika Moyo Baada ya Roma Kuaga Coppa Italia"
Baada ya mechi hiyo, AS Roma atasafiri kwenda ugenini kucheza mchezo wa ligi dhidi yaTorino tena ambaye amemuondosha kwenye michuano ya Coppa Italia. Je vijana wa Gasperini watafanyaje?

Leo hii endelea kufanya ubashiri na Meridianbet wakali wa ubashiri Tanzania kwani ODDS KUBWA na machaguo zaidi ya 1000 yapo hapa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.