Uwanjani leo kuna jumla ya mechi nne kwenye Kombe la Dunia na kocha Carlos Queiroz atakuwa akikiongoza kikosi chake katika kusaka taji hilo na mechi yao leo ni dhidi ya taifa la Ureno.
Kocha huyu atakuwa akimtegemea mchezaji staa Sardar Azmoun wakati nchi hiyo ikikipiga mechi yake baada ya kuwa ni mara ya nne kwao kushiriki kwenye fainali 6 zilizopita lakini ushindi wao pekee ulikuwa ni dhidi ya USA. Hii ilikuwa ni mwaka 1998 walipokutana.
Iran waliweza kushinda mchezo wao wa mwisho kufuzu kwenye Kundi wakicheza dhidi ya Korea Kusini na katika gemu zilizopita wameshinda mmoja dhidi ya Morocco na kupigwa na Hispania. Leo wataweza kushinda na kuweka matumaini ya kufanikiwa zaidi au wataharibu?


Ester jackson
Asee lilikuwa bonge la pambano
Povel
Gud news
Zeiyana
Siwezi kusahau ule mtanange
Furahav
Ureno iko sawa.