Mshambuliaji wa Juventus, Federico Chiesa anasisitiza Massimiliano Allegri anataka Bianconeri icheze ‘soka la kisasa’.

Mshambuliaji huyo wa Italia alizungumza na DAZN kufuatia ushindi wa 1-0 wa Juventus dhidi ya Lecce Jumanne. Bianconeri walizinduka mara baada ya kupoteza kwa mabao 4-2 dhidi ya Sassuolo. Chiesa aliulizwa ikiwa kushindwa kwa Reggio Emilia kumeathiri timu dhidi ya Lecce.
“Labda katika kipindi cha kwanza, tulikuwa tumecheza siku mbili au tatu zilizopita,”. Tulichambua mchezo dhidi ya Sassuolo na tulifanya vyema katika dakika 20 za mwanzo. Tunataka kupanda juu na kucheza soka la kisasa jinsi kocha anavyotaka. Kulikuwa na makosa ya mtu binafsi dhidi ya Sassuolo, lakini tulimshinda Lecce kwa matokeo mazuri katika kipindi cha pili.”|Alisema Chiesa
Sio mara ya kwanza msimu huu Chiesa kusema ni lazima Juventus wacheze soka la kushambulia.

Chiesa amekuwa akicheza kama mshambuliaji wa kati msimu huu, kwa hivyo kuna tofauti gani ikilinganishwa na nafasi ya winga?
“Hakika, kuna mabadiliko kwa sababu ninapocheza kwa upana naweza kwenda moja dhidi ya moja, wakati, ninapocheza katikati, kuna wapinzani zaidi mbele yangu. Ni sehemu ya uboreshaji ninaohitaji kufanya. Kocha anataka. Ananiambia nicheze karibu na lango na nadhani ninatoa uaminifu na mwanzo huu wa msimu.”
Mshambuliaji huyo amesema kuwa alicheza na Vlahovic huko Fiorentina kwahivyo wako sawa, lakini Milik Kean na hata Yildiz ambaye anaimarika ni wachezaji wazuri ambao wanaweza kuwasaidia pia.

Wakati Alessandro Matri, mmoja wa wachambuzi wa DAZN na mshambuliaji wa zamani wa Juventus alibainisha kuwa mtindo wa Chiesa wa kupiga mashuti ni sawa na baba yake Enrico, Federico alijibu akitabasamu. “Ndio, ni kweli, lakini hakuwahi kuniambia siri yake.”
Chiesa mwenye miaka 25, amefunga mabao manne katika mechi sita katika michuano yote msimu huu na mkataba wake na wababe hao wa Serie A unamalizika Juni 2025.

