Klabu ya Juventus yazidi kung’ara huko Serie A baada ya kuendelea kuonyesha kiwango kizuri na kuwafanya wakae nafasi ya 4 kwenye msimamo Serie A baada ya kuwatandika Hellas Verona kwa bao 1-0 wakiwa ugenini.

Mechi inayofuata ya Juventus watakipiga dhidi ya Lazio ambaye yupo nafasi ya pili baada ya kupata ushindi hapo jana . Mechi yao inatarajiwa kupigwa siku ya umapili, kabla ya mapumziko ya Kombe la Dunia.
Hivyo mpaka sasa vijana hao wa Massimiliano Allegri wapo nafasi hiyo wakiwakimbiza Atalanta na Inter Milan ambao wako tayari kwa pambano lao zito wikendi hii, wakati viongozi wa ligi Napoli wanaweza kuendeleza wimbi lao la moto wakiwa nyumbani kuwakaribisha Udinese.

Kwingineko mabingwa watetezi AC Milan wanawakaribisha Fiorentina katika dimba la San Siro huku wakiwa wamezidiwa pointi 8 na vijana wa Luciano Spalletti, wakati huo huo Roma ya Mourinho watataka kufufua hali yao ya kigugumizi kwa kutaka ushindi dhidi ya Torino.
Juventus na Lazio wanajivunia safu mbili bora za ulinzi kwenye ligi msimu huu na wingi wa ubora katika safu zao unaonyesha kuwa hili litakuwa pambano la kuvutia kabla ya kwenda Kombe la Dunia.

Kocha wa Juve Allegri anatumaini kwamba Moise Kean ataendeleza kiwango chake kizuri alichokionyesha mechi iliyopita dhidi ya Verona ambapo mchezaji huyo ana miaka 22 mpaka sasa.

Ulishawahi kuwaza kuwa rubani wa maisha yako!! Kuwa rubani wa mchezo pendwa wa Aviator wa kasino mtandaoni. Aviator bonanza inazidi kutoa michongo ya mkwanja kwenye nyumba ya mabingwa. Unarusha ndege yako na unashinda, kuwa rubani wa kujivunia kwa kuibuka na mkwanja leo.
BONYEZA HAPA

