Staa wa zamani wa klabu ya Inter Milan na timu ya taifa ya Uholanzi Wesley Sneijder amesema anaamini kocha wa klabu ya As Roma Mreno Jose Mourinho bado ni namba moja duniani.
Jose Mourinho ambaye ametimiza miaka 60 katika maisha yake siku ya leo akiwa ndani ya klabu ya Roma, Huku akifanikiwa kuisaidia klabu hiyo kushinda taji la Uefa Conferernce League mwaka 2022 ambapo ilikua ni baada ya kupita miaka minggi bila klabu hiyo kushinda taji lolote.
Baada ya kushinda taji la Uefa Conference League mwaka jana akiwa na klabu ya AS Roma alifanikiwa kuweka ekodi kwa kubeba kila taji ambalo lipo chini ya shirikisho la soka ulaya Uefa, Kwani alifanikiwa kubeba taji la ligi ya mabingwa ulaya akiwa na Fc Porto 2004, pamoja Inter Milan 2010, Uefa Europa 2017 akiwa na Manchester United na Uefa Conference League mwaka 2022 akiwa na As Roma.
Sneijder anamkumbuka zaidi Mourinho akiwa kama kocha wake ndani ya klabu ya Inter Milan mwaka 2010 wakifanikiwa kubeba mataji matatu ndani ya msimu mmoja, Huku staa huyo akiutafsiri kama msimu bora zaidi kwenye maisha yake ya soka na ndio sababu anaamini kocha huyo ni namba moja kwake.
Gwiji Wesley Sneijder ni miongoni mwa wachezaji waliunda Inter Milan dume kabisa nchini ya kocha ya kocha Jose Mourinho na kufanikiwa kushinda mataji matatu ndani ya msimu mmoja ambayo ni Ligi ya mabingwa barani ulaya, Ligi kuu ya Italia Serie A, na Copa Italia.

