Zhang Athibitisha Kuwa Inter Haiuzwi

Rais wa Inter Steven Zhang amesisitiza kujitolea kwa Suning kwa klabu ni kwa muda mrefu huku Nerazzurri wakithibitisha mapato yao yakiongezeka kwa takriban €75m mnamo 2021-22.

 

Zhang Athibitisha Kuwa Inter Haiuzwi

Mkutano wa wanahisa wa klabu umefanyika katika makao makuu ya klabu na kuidhinisha matokeo ya kifedha ya 2021-22. Inter iliongeza mapato kwa €75m katika mwaka wa fedha unaoisha Juni 2022, na kupata €439.6m ikilinganishwa na €364m mwaka wa 2020-21.

Wababe hao wa Serie A pia walipunguza gharama kwa takriban €140m, kutoka hasara ya €245.6m mnamo 2020-21 hadi €105m mwaka jana.

Rais wa Inter Steven Zhang alifungua mkutano huo kwa hotuba kuthibitisha kujitolea kwa muda mrefu kwa Suning. Alimshukuru mkurugenzi Beppe Marotta akisema kwamba kazi yake ilisaidia Inter kubaki katika kiwango cha juu cha soka ya Italia na Ulaya, na kujadili changamoto za siku zijazo.

Zhang Athibitisha Kuwa Inter Haiuzwi

Mmiliki wa klabu hiyo tayari alikuwa amekanusha kuwa klabu hiyo ilikuwa inauzwa Jumatano baada ya Inter kushinda 4-0 dhidi ya Viktoria Plzen kwenye Ligi ya Mabingwa.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.