Klabu ya Leicester City wamemtumbua aliyekuwa meneja wa klabu Claude Puel hiyo baada ya kuonekana ameshindwa kuwapatia matokeo ambayo wanayatarajia au kuyahitaji zaidi katika kipindi hiki.
Meneja huyu anaripotiwa kuwa alikuwa kwenye uangalizi kama angeweza kuboresha matokeo zaidi lakini kichapo cha bao 4-1 kutoka kwa Crystal Palace kumemfanya awe hana bahati klabuni hapo na kukutana na rungu la kutumbuliwa.
Mashabiki wengi wanaripotiwa kutofurahishwa na mwenendo wa matokeo wakiwa wameshindwa kupata ushindi wowote kwenye gemu ya nyumbani kwa mwaka 2019 huku wakipata ushindi mara moja tu katika gemu zao 9 za ugenini za mashindano yote.
Klabu hii imeamuua kufanya mabadiliko kujaribu kuokoa Jahazi. Rungu la kutumbuliwa limewapitia meneja wa Tuchel kama Mkufunzi mkuu wa klabu hiyo na msaidizi wake Jacky Bonnevay na wote wametakiwa heri ya kusepa klab uni hapo.
Mike Stowell and Adam Sadler wamechukua majukumu ya mda ya ukufunzi wa kikosi cha kwanza wakati klabu ikiwa kwenye mawindo ya kuwapata viongozi wapya wa kudumu.


Shafii
Duh sio poa
Furahav
Hatari sana.
Povel tz
Duh noma sana