Nyota hao ni Lamine Moro, Bernard Morrison, Juma Abdul, Haruna Niyonzima, Ditram Nchimbi, Said Juma, Patrick Sibomana na Papy Tshishimbi ni wachezaji ambao wanatazamwa kwa uangalizi zaidi.

Mbeligiji huyu anataka kuhakikisha Wananchi wanabaki kwenye kiwango chao, pamoja na ligi kusimamishwa.
“Nafatilia maendeleo ya kila mchezaji akiwa nyumbani, kwasababu nataka timu iwe na muonekano mzuri mechi zikirejea,” Eymael amesema.
“Ninawatazama sana, Moro, Morrison, Juma, Niyonzima, Ditram, Said, Sibomana, na Papy kwasababu zangu za kiufundi. Nataka kuona wakifata maelekezo waliyopewa na benchi la ufundi. Lakini kila siku napata repoti ya kila mchezaji.”
“Tunataka watunze hali zao kisaikolojia na fizikia, haitafurahisha ukiwakuta wachezaji wanashepu mbaya. Timu inatakiwa iwe tayari kucheza muda wowote na ndio maana tunaendelea kujiandaa.”
Yanga kwasasa wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi wakuwa na alama 51.

