Rais wa Barcelona Joan Laporta amesisitiza kumweka Lionel Messi katika klabu hiyo mwaka 2021 ilikuwa haiwezekani kwa sababu klabu hiyo ilikuwa imeyumba kifedha.

 

Laporta Anasisitiza Messi Asingeweza Kusalia Barca Kwani Klabu Ilikuwa Inayumba

Baada ya kupitia akademi ya Barca, kuondoka kwa Messi kulimaliza ushirika wa miaka 21 na kuangazia uzito wa maswala ya kiuchumi ya kilabu.

Mkataba wa Messi ulimalizika mwishoni mwa msimu wa 2020-21, na ingawa kiufundi alikua mchezaji huru, ilidhaniwa kuwa Barca wangemsajili tena kwa mkataba mpya mara tu chumba kitakapowekwa kwenye bajeti.

Lakini Barcelona ambao madeni yao yalikuwa euro bilioni 1.35 mnamo Agosti 2021 – walipunguza kiwango cha mshahara wao wa LaLiga kwa euro milioni 280 kabla ya kampeni ya 2021-22 kama matokeo ya shida zao za kifedha.

Laporta Anasisitiza Messi Asingeweza Kusalia Barca Kwani Klabu Ilikuwa Inayumba

Kwa hivyo, hata ikiwa imeripotiwa kupunguzwa kwa mishahara kwa asilimia 50, Barca bado hawakuweza kumudu kumsaini Messi kwa mkataba mpya, na sheria ya uajiri ya Uhispania inakataza waajiri kupunguza mishahara zaidi ya asilimia 50.

Laporta amesema kuwa; “Ilinibidi kuiweka Barca mbele ya mchezaji bora zaidi katika historia ya soka. Katika nyakati hizo za uharibifu wa kifedha sikuweza kubaki naye. Nadhani lilikuwa jambo bora zaidi kwa klabu.”

Bila shaka, Messi anaendelea kuhusishwa na kurejea Barca huku kandarasi yake ya Paris Saint-Germain ikitarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu. Vile vile, ripoti zinaonyesha Messi tayari amekubali kuongeza muda na PSG, tangazo hilo lilicheleweshwa tu na ushiriki wake na likizo baada ya kutwaa Kombe la Dunia.

Laporta Anasisitiza Messi Asingeweza Kusalia Barca Kwani Klabu Ilikuwa Inayumba

Laporta ameongeza kuwa anapendelea kutozungumza juu ya Leo kwasbabu ni mchezaji wa PSG, kwani wakati huo kama angezungumza juu yake angeleta makombora ambayo yanatoka kila mahali.

 “Tunazingatia wachezaji ambao ni wetu. Leo daima atakuwa sehemu ya nembo yetu, na ningependa awe na mwisho tofauti na ule aliokuwa nao.”

JIBU

Tafadhali andika maoni yako
Tafadhali andika jina lako hapa