Mshambuliaji wa klabu ya Fc Barcelona Roberto Lewandowski anaamini staa wa klabu ya PSG na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi yupo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kushinda tuzo ya Ballon Dor mwaka huu 2022.
Staa Lionel ambaye amekua kwenye kiwango bora sana na klabu yake ya PSG akifanikiwa kuhusika kwenye mabao mengi msimu huu, Huku ikiwa tofauti sana na msimu uliomalizika ambapo mchezaji huyo alikua na msimu mbaya ndani ya klabu hiyo.
Mshambuliaji Lewandowski anaamini Messi yupo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa dunia maarufu kama Ballon Dor kutokana na kiwango bora alichokionesha kwenye michuano ya kombe la dunia mwaka huu nchini Qatar.
Lionel Messi amefanikiwa kuhakikisha anaiwezesha timu yake ya taifa ya Argentina inashinda taji la kombe la dunia nchini Qatar, Huku yeye akiwa na kiwango bora sana na akifanikiwa kushinda tuzo ya mchezaji bora wa michuano hiyo mwaka huu.
Staa Lewandowski anaamini kipimo kikubwa cha mchezaji kupewa tuzo ya mchezaji bora wa dunia itakua michuano ya kombe la dunia, Hivo anaamini kwa kiwango alichoonesha Lionel Messi kwenye michuano hiyo ni wazi kabisa yupo kwenye nafasi nzuri zaidi ya kutwaa tuzo yake ya nane ya Ballon Dor.

