Pigo kwa Real Madrid: David Alaba Aumia, Atakosa Mechi ya Celta Vigo

Klabu ya Real Madrid imepata pigo jingine kuelekea mchezo wao wa ugenini dhidi ya Celta Vigo baada ya beki wao tegemeo David Alaba kuumia misuli ya mguu, hali itakayomfanya akose michezo ya wiki hii. Taarifa kutoka ndani ya klabu zinaeleza kuwa beki huyo wa kimataifa wa Austria anahitaji muda wa kupumzika na matibabu ili kurejea katika kiwango chake bora.

Mbali na hao, mabeki Éder Militão na kiungo Dani Ceballos pia bado hawajawa tayari kurejea uwanjani kutokana na changamoto za kiafya. Hali hii inalazimisha benchi la ufundi kufanya marekebisho ya kikosi kabla ya mchezo huo muhimu wa ligi. Katika upande mwingine, Real Madrid pia itawakosa wachezaji watatu ambao hawatacheza kutokana na kutumikia adhabu za kinidhamu. Wachezaji hao ni Dean Huijsen, Álvaro Carreras pamoja na Franco Mastantuono ambao hawatakuwa sehemu ya kikosi katika mechi hiyo.

Pigo kwa Real Madrid: David Alaba Aumia, Atakosa Mechi ya Celta Vigo

Kutokana na hali hiyo, Real Madrid italazimika kutumia mbinu mbadala na kuwapa nafasi baadhi ya wachezaji wengine ili kujaribu kupata matokeo mazuri dhidi ya Celta Vigo. Mashabiki wa klabu hiyo sasa wanasubiri kuona namna timu yao itakavyokabiliana na changamoto ya majeraha na adhabu katika kipindi hiki muhimu cha msimu.

Pigo kwa Real Madrid: David Alaba Aumia, Atakosa Mechi ya Celta Vigo

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.