Mshambuliaji hatari wa Borussia Dortmund, Serhou Guirassy, anaripotiwa kuwa tayari ameweka wazi nia yake ya kuondoka klabuni mwishoni mwa msimu. Licha ya kuwa na mkataba hadi 2028, nyota huyo wa Guinea anataka changamoto mpya, na tayari klabu kadhaa zimeanza kuonyesha nia ya kumsajili.

Inaelezwa kuwa Guirassy ana kipengele cha kuachiliwa kwa euro milioni 35 kitakachoanza kufanya kazi majira ya joto, lakini kwa masharti maalum, kikilenga vilabu vikubwa kama Real Madrid, FC Barcelona, Manchester United, Manchester City, Arsenal, Chelsea na Liverpool. Hii inaacha mustakabali wake wazi kwa dili kubwa.
Vilabu kama AC Milan na Fenerbahçe vinaonekana kuwa mstari wa mbele, huku pia timu za Premier League na Saudi Arabia zikitajwa kuvutiwa naye. Ingawa Saudi Arabia ilionekana kuwa chaguo la kifedha, sasa inaelezwa kuwa si kipaumbele chake kikuu.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande wa Dortmund, hili ni pigo kubwa kwani Guirassy ndiye kinara wa mabao. Hivyo, uongozi wa klabu tayari unaangalia mbadala wake, huku majina mawili yakitajwa zaidi, Nicolo Tresoldi na Fisnik Asllani.

Tresoldi anaonekana kuwa chaguo la bei nafuu bei yake ikiwa ni euro milioni 25–30 na tayari ameonyesha kiwango bora, wakati Asllani naye ana kipengele cha euro milioni 30 lakini anakabiliwa na ushindani kutoka FC Barcelona, ambao nao wanamfuatilia kwa karibu.

