Kocha mkuu wa klabu ya Newcastle United Eddie Howe amesema kuwa haoni haja ya kulalamika kutokana na kile kitendo kilitokea katika mechi yao iliyopita dhidi ya Liverpool ambapo walikuwa wageni wa mchezo huo.

Kauli hiyo inatokana na kitendo cha refa wa mchezo huo kuongeza dakika 8 kitu ambacho
kilifanya wafungwe bao ambalo liliifanya Liverpool aondoke na alama tatu za muhimu. ambapo bao hilo la kuipa Majogoo alama tatu lilifungwa na Fabio Carvalho.
Baada ya kupoteza mchezo huo kocha wa timu hiyo Howe alisema kuwa haoni umuhimu wa kufanya hivyo kwani hata wakilalamika hawaoni faida yoyote kwenye kulalamika kwani watawekeza nguvu kwenye kitu chanya na chenye thamani zaidi, na hiyo itakuwa kwa wachezaji wangu kila wakati.

Newcastle ambayo msimu uliopita imenunuliwa na Saudi Arabia’s Public Investment Fund na washirika wengine wameifanya timu hiyo kunusurika kushuka daraja na kumalizia msimu wakiwa nafasi nzuri, Lakini pia wamefanya usajili mzuri msimu huu akiwemo nyota wa zamani wa Real Sociedad na timu ya Taifa ya Uswis Alexander Isak ambaye mechi yake ya kwanza tu dhidi ya Liverpool alitupia bao.

