Kocha wa Newcastle United Eddie Howe ameshinda tuzo ya kocha bora wa mwezi wa pili inayotolewa na wadhamini wa EPL Barclays baada ya kuiongoza timu hiyo kushinda michezo mitatu na sare moja amewapiku makocha Ralph Hasenhüttl wa Southampton, Jürgen Klopp wa Liverpool na Mikel Arteta wa Arsenal kwenye kinyang’anyiro hicho.
Hii inakuwa mara ya nne kocha huyo kutwaa tuzo hiyo aliwahi kushinda mwezi Machi 2017, Januari 2018 na Oktoba 2018 wakati alipokuwa kocha wa klabu ya AFC Bournermouth.
Newcastle ilizifunga Everton, Aston Villa na Brentford na kutoa sare na West Ham mwezi uliyopita na kwa mwezi huu Machi tayari ameshinda mechi mbili.
“Nimeshinda kweli, kwa niaba ya kila mtu anayehusika na klabu, wafanyakazi, wachezaji wamiliki. “Mimi ni mtu ninaye simama tu kwenye kuiongoza lakini kuna kazi nyingi inayofanyika nyuma ya kila kitu. Alisema kocha huyo wa Magpies
“Najisikia vizuri asante kwa kila mtu.
Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000 katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.