Baada ya kutolewa kwenye Michuano ya Ulaya – UEFA kwa faida ya goli la ugenini dhidi ya Olympique Lyonnais. Kocha wa Juventus – Maurizio Sarri anadhani timu yake imelaaniwa katika michuano hiyo.
Katika mchezo wa kwanza, Lyon waliibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Juventus na hivyo kuifanya mechi yao ya marudiano kuwa ngumu zaidi. Juventus waliihitaji ushindi wa zaidi ya goli 2 ili kufuzu hatua ya robo fainali ya Michuano ya Ulaya – UEFA.

Magoli mawili ya Cristiano Ronaldo hayakutosha kuivusha Juventus kwenda hatua ya robo fainali. Mshambuliaji Mephis Depay alikuwa wa kwanza kuzitingisha nyavu za Juventus na hivyo kuizamisha kabisa timu ya Juventus.
Akizungumza baada ya mchezo huo, Sarri amesema ” tumetolewa kwenye michuano ambayo tumeshinda michezo 6 kati ya 8 tuliyocheza, tumesuluhu 1 na kupoteza 1. Hii inamaanisha katika michezo 8 tumekusanya pointi 19″

“Kama kungekua na msimamo wa Michuano ya UEFA, tungekuwa wa kwanza au wa pili, lakini tumetoka. Ndio maana ninajisikia vibaya sana, inanifanya nielewe kwamba Juventus tumelaaniwa kwenye michuano hii.”
“Nisingekuwa na uchungu, ningetoka kwenye hii mechi nikiwa na uso wenye tabasamu kwa sababu nimewaona vijana wakicheza vizuri. Wamejitahidi kwa kila walichoweza kukitoa uwanjani kwa moyo wao wote mpaka mwisho wa mchezo, nimefurahi kwa hilo.”
Lyon na Juventus wote walipatiwa penati za kutatanisha, Ronaldo na Depay walitumia fursa hizo kufunga magoli. Sarri ameonekana kutofurahishwa na penati waliyopewa Lyon na kwamba kwake yeye haikuwa sahihi.

Sarri amesema ” Tulicheza vizuri katika mchezo ambao tulitokea nyuma ili kupata matokeo. Tulijikuta tumefungwa kwa sababu ya penati ya kijinga. Kwa maoni yangu wasingepaswa hata kufika kwenye boksi kwa sababu ya madhambi aliyofanyiwa Gonzalo Higuain. Ile penati ni mjadala.”
“Refa hakuonesha uwezo wake katika nafasi kama ile. Kwa sisi kufungwa lile goli moja, kwetu ni kama tulifungwa magoli mawili. Tulikuwa vizuri kwasababu tulibadilisha matokeo lakini tulitumia nguvu kubwa sana”.

“Tulipata nafasi mbili au tatu za kufunga magoli dakika za mwisho kwa vichwa vya Ronaldo, Higuain nadhani na Leonardo Bonucci, nadhani tulikuwa karibu kufuzu. Kama tunapaswa kulaumu, basi tunapaswa kujilaumu kwa mchezo wetu wa kipindi cha kwanza tulipokuwa Lyon. Katika viwango hivi, ni kitu unapaswa kulipia”.
Kwa ushindi huu wa Lyon, unaifanya Juventus kuendelea kusubiri kubeba kombe la UEFA tangu mwaka 1996.
Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.


Mwanahamisi
Asante kwa taarifa
Adelta
Asante kwa makala nzuri
#meridianbettz
Zeiyana
Ni kweli juventus walijitaidi sana ila ndio hivyo tena bahati haikuwa kwao..!wasimame wajipange upya
felister
Sio laana ni bahati tu haikuwa upande wao
JULIANA
Asante kwataharifa
Adelta
Asante kwa makala nzuri
Mwanahamisi
Gud news
Povel
Kibibi kizee cha Turin inabid wajenge timu upya maana kila msimu wanaonekana wanaishia pale pale
magdalena
juve walifanya kila jitihada lakini hazikufanikiwa chochote
Issa
Lyon walijihakikishia nafasi toka mwanzo alafu walikua na hali ya ushindi ingawaj juve walipigana pia
Lydia Emmanuel Magoti
Juve siolana ilandio mchezo walizidiwa kwaio wajipange sasa
Rehema
Asante kwa makala mzur
Sadick
Juventus imeweka nguvu nyingi kwenye Kombe hili lakini mara zote mambo yamekuwa magumu kwao. Inatakiwa kusajiri wachezaji watakaowezesha kufikia lengo hilo#meridianbettz
aisha
Kila kitu kinaenda kwa riziki haikuwa riziki yao
Amiri Kayera
Akuna UEFA ngum sanaa
Nasra
Wajipange tu
Dorophina
Walijitahidi sana juve lakini ndo ivyo haikuwa bahati yao
Mwajumah
Si laana ila bahat haikuwa upande wao
Caroline
Hapana sio laana bc tu wakati haujafika
Furahav
Juve wana wachezaji wazuri ila hawajitumi.
Fatina mfingi
Wajipange upya
Tatu
Juve kwa msimu huu wamebologa labda wajipange mwakani
Hope mwaikuka
Pambanen
Ernest Kimeru
Kiukweli Lyon wamekuwa na bahati zaidi ya Juventus
Gabriel
Nice update 👍
Shafii
Inapaswa watambue kwamba mpira Una mambo matatu na wahenga wanasema asiye kubali kushindwa sio mshindani.
farida ahmadi
Kikubwa kujiweka sawa na kujipanga vzr kwenye msimu hujao
Saupha mohamed
Wajipange msimu ujao
Fatuma kasomo
Asante kwataarifa
Frank
Huyu mzee kweli anazeeka na kiburi
Latifa juma mohamed
Asante kwa taarifa
David Pere
Yawezekana ni kweli maana kila msimu wanatolewa mapema na ukiangalia Wana timu nzuri tu
Genia Sikaluzwe
Wajipange upya
Ester jackson
Si bahati yao mana kutoshinda au kutolewa sio kwamba wamelaaniwa bado zamu yao mbona Liverpool walikaa miaka mingi bila kupata ubigwa sasa wanaushehekea ipo siku nao watavunja ukimnywa wao
Khadija
Juve wapo vizuri sana hila hawajitumi#meridianbettz
Samiah
Juve wapo vzr
Sabrina
Duuuh wajipange tu watakua sawa
Omary lukumbi
Safi sana sarri umezungumza kijasir sana kama kocha na kuto kuwavunja moto wachezaj wako ingekua kama ndio kocha wa yangawalio mtimua basi nahisi ange watukana wachezaj au hata kuwakashfu kuwa walibeteka
warda
Hii ilimuuma sana CR7