Lewandowski Aingia Klabu Maalum Mabingwa wa Mabao Ulaya

Robert Lewandowski ameandika historia mpya barani Ulaya baada ya kujiunga na klabu adimu ya washambuliaji waliovuka mabao 20 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya wakiwa na zaidi ya klabu moja. Mshambuliaji huyo wa Poland alikuwa miongoni mwa nyota wa Barcelona katika ushindi wa kusisimua wa mabao 4–2 dhidi ya Slavia Prague, akifungua ukurasa wake wa mabao kwenye msimu wa Ligi ya Mabingwa 2025/26.

Katika mchezo huo, Lewandowski alionyesha kwa nini bado anahesabiwa miongoni mwa washambuliaji bora barani Ulaya. Alijikuta akihusika pande zote mbili za uwanja, lakini bao lake muhimu ndilo lililomfikisha kwenye jumla ya mabao 20 ya Ligi ya Mabingwa akiwa na Barcelona. Mafanikio hayo yanakuja baada ya nyota huyo kufunga mabao 69 ya michuano hiyo alipokuwa Bayern Munich kabla ya kujiunga na Barca mwaka 2022.

Lewandowski Aingia Klabu Maalum Mabingwa wa Mabao Ulaya

Kwa kufikia rekodi hiyo, Lewandowski sasa yuko kwenye orodha fupi ya mastaa wakubwa wa soka duniani. Ni wachezaji watatu pekee waliowahi kufunga mabao 20 au zaidi ya Ligi ya Mabingwa wakiwa na klabu mbili tofauti, Cristiano Ronaldo (Manchester United na Real Madrid), Harry Kane (Tottenham na Bayern Munich) pamoja na Neymar (Barcelona na Paris Saint-Germain). Sasa jina la Lewandowski limeongezwa rasmi kwenye historia hiyo ya heshima.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Zaidi ya hapo, bao lake dhidi ya Slavia Prague limemhakikishia Lewandowski kufunga katika msimu wa 15 mfululizo wa Ligi ya Mabingwa. Rekodi hiyo inamweka karibu na vigogo wa soka duniani, huku Cristiano Ronaldo akiwa na misimu 16 mfululizo, na Lionel Messi pamoja na Karim Benzema wakiongoza kwa misimu 18 kila mmoja.

Lewandowski Aingia Klabu Maalum Mabingwa wa Mabao Ulaya

Akizungumza baada ya mchezo, Lewandowski alifichua furaha yake baada ya hatimaye kufungua akaunti yake ya mabao msimu huu, akisema; “Hatimaye bao la kwanza limepatikana. Natumaini sasa itakuwa rahisi zaidi.” Tangu afunge bao lake la kwanza la Ligi ya Mabingwa mwaka 2011 akiwa Borussia Dortmund, Lewandowski ameendelea kudumisha kiwango cha juu ajabu. Hadi sasa ana mabao 114 kwenye mashindano ya UEFA, akiwa wa tatu kwenye orodha ya wafungaji bora wa muda wote, nyuma ya Ronaldo (145) na Messi (132).

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.