Klabu ya Liverpool wamejiandaa kutumia pesa nyingi kumsajili winga wa Barcelona Ousmane Dembele kama mbadala wa Sadio Mane katika majira yajayo ya kiangazi.
Umekuwa msimu wa kukatisha tamaa kwa Mane, ambaye amefunga mabao 12 tu kwenye mashindano yote na matano tu tangu mwanzoni mwa mwaka wakati kikosi cha Jurgen Klopp kikitolewa kwenye mashindano kwa kila kombe.

Ripoti zinaonesha kwamba Liverpool inafikiria kumtengea pesa mchezaji huyo wa kimataifa wa Senegal, 29, katika msimu huu wa joto licha ya mkataba wake kuwa bado na miaka miwili kumaliza.
Kulingana na ripoti za Fichajes.net huko Uhispania, Dembele ndiye mtu anayekusudiwa kuchukua nafasi yake.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa, 23, amebakiza mwaka mmoja tu kwenye kandarasi yake ya Barcelona lakini bado hajasaini nyongeza aliyopewa.
Kila mtu ana namba zake za bahati, Meridianbet tunatambua namba zinaweza kukufanya milionea leo. Jilipe kwa namba zako za bahati kila baada ya dakika tano.



Adelta
Tuone itakuwaje
Venerose
Jambo jema
Sarah
Habari nzuri
warda
Hawa liverpool kila siku wanawaza kusajili tu