Klabu ya Liverpool imeongeza nguvu zaidi kwenye harakati za kuwania saini ya winga wa Real Madrid na Hispania, Marco Asensio, 25, kuelekea dirisha lijalo la majira baridi linalofunguliwa Januari 2022.

Asensio amekuwa akihusishwa kuondoka Real Madrid tangu dirisha lililopita kwa sababu hajisikii furaha kuendelea kusalia kwenye viunga hivyo vilivyompa jina kubwa katika soka.
Mkataba wa sasa wa supastaa huyo unamalizika 2023 na msimu huu amecheza mechi saba za michuano yote ambapo amefanikiwa kufunga mabao matatu.
Madrid haionekani kuwa na mpango wa kumzuia ikiwa ofa inayohitaji itawasilishwa mezani kwani Asensio mwenyewe amewaambia mabosi kwamba anahitaji changamoto mpya, Liverpool wanaongoza kupata saini ya mchezaji huyo kwasasa.
SPACE SPIN NA MERIDIANBET.
Ni Mabingwa pekee Meridianbet wanakupa nafasi ya kushinda zaidi na mchezo wa Space Spin katika kasino bomba za meridianbet. Ni wakati wa kufurahia na kutengeza mkwanja bila kuwaza.


