Kocha mkuu wa klabu ya Everton Rafa Benitez amethibitisha kuwa beki wake wa kushoto Lucas Digne ameomba kuondola kwenye klabu hiyo ambapo hajacheza tokea mwezi Disemba mwaka jana.
hakuna maelezo zaidi yaliotelwa kwa kocha huyo kwanini beki huyo ameomba kuondoka, lakini Benitez anadhani kuwa Lucas Digne ameweka maslai yake zaidi kuliko klabu.

Benitez alisema “nimekuwa na mazungumzo nae mara kadhaa, aliniambia nini anafikilia, nini unatarajia ikiwa mchezaji anakwambia kuwa kuwa haitaji tena kuwa hapa.
“Nadhani alikuwa muwazi, nataka kuuliza swali kwa shabiki au mchezaji yeyeto wa zamani, nini Peter Reid atasema ikiwa mchezaji hataki kuwa hapa? aliniambia anachofiklia, sasa mnategemea kocha afanyaje?.
“Sina cha kueleza, sisi ni wataalamu wa soka, tunalipwa pesa nyingi ili kufanya kazi yetu, kwenye mpira wakisasa, huenda vipaumbele vimebadilika na watu wanajifikilia wenyewe kuliko timu.”
Lucas Digne hivi karibuni amekuwa akihusishwa na vilabu vya Chelsea, Newcastle na West Ham, Everton kwa sasa haina mwendelezo mzuri kwenye ligi kuu ya Uingereza, kwenye msimamo wanashika nafasi 15 wakitofautiana pointi nane tu na timu zilizopo kwenye hatari ya kushuka daraja.
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


