Lyon Wawaacha Hoi City, Watinga nusu Fainali UEFA.


Manchester City ilionekana kuwa kwenye mkondo sasa wa kushinda mechi hiyo baada ya bao la Kevin De Bruyne katikati ya kipindi cha pili kufuta bao la ufunguzi la Maxwel Cornet katika kipindi cha kwanza.

Moussa Dembele aliingia uwanjani kama mchezaji wa akiba na kufunga mabao mawili ya dakika za mwisho wakati Lyon ikisababisha mshangao mwingine wa Ligi ya Mabingwa, kwa kuiondoa Manchester City ya Pep Guardiola.

 

Lyon Wawaacha Hoi City, Watinga nusu Fainali UEFA.

Kinyume na matarajio yote, timu iliyomaliza katika nafasi ya saba katika msimu wa kandanda la Ufaransa, na ambayo ilikuwa imecheza mechi mbili pekee za ushindani tangu mapema Machi, sasa itacheza katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Jumatano dhidi ya Bayern Munich.

Hiyo bila shaka ni hatua kubwa kwa timu hiyo ya Rudi Garcia na lakini pia hakuna aliyetarajia kuwa wangewaondoa Juventus katika duru ya mwisho, achia mbali kuwaondoa City katika hatua ya robo fainali.

“Bado tuko mashindanoni, kumaanisha kuwa tuna timu nzuri,” Mshambuliaji wa zamani wa Celtic Dembele aliiambia televisheni ya Ufaransa ya RMC Sport. “Tunazungumzia mechi moja baada ya nyingine, hatutajisahau. Tutajaribu kuwa tayari kuvaana na Bayern.

Timu hiyo ya Guardiola ilikuwa imepewa onyo na Lyon, kwa kushindwa nyumbani na kisha kutoka sare ugenini dhidi ya klabu hiyo ya Ufaransa katika Ligi ya Mabingwa msimu uliopita. Lakini hiyo ilikuwa karibu miaka miwili iliyopita na Lyon imepoteza wachezaji kadhaa muhimu tangu wakati huo.

 

Lyon Wawaacha Hoi City, Watinga nusu Fainali UEFA.
 

Matokeo haya, siku moja baada ya Bayern kuibomoa Barcelona 8 – 2, ni mshtuko mkubwa na pigo kubwa kwa malengo ya City chini ya Guardiola.

Subira yao ya kushinda Kombe la Ulaya itaendelea, hii ikiwa ni mara ya tatu mfululizo kuondolewa katika robo fainali. “Hivyo ndivyo ilivyo. Labda siku moja tutaweza kupenya katika robo fainali. Hatujaweza kufanya hivyo sasa, na hawa vijana wazuri kweli, lakini tutajaribu tena katika siku za usoni.” Alisema Guardiola.


Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.

Soma zaidi

39 Komentara

    Oky tuwape hongera lyon kwa ushindi lakini huo ndio mpira hakuna cha kushangaa

    Jibu

    Safi sana Lyon

    Jibu

    Wahenga walishasema kwamba mpira unadunda hivyo unaweza kudunda kuelekea upande wowote na ndivyo ilivyokuwa. Hongera Kocha Garcia kwa mbinu za ushindi#meridianbettz

    Jibu

    Hongera sana. Lyon

    Jibu

    Hongera sana Lyon ingawaje man city walishambuliwa sana lakini mliwazidi triki katika kupachika magoli

    Jibu

    Walijitahidi sana Lyon walicheza kwa kujiami na kushamulia kwa kushtukiza walifanya poa sana walilinda goli lao na walifanikiwa kuwatoa city

    Jibu

    Man City walijiamini Sana hii mechi bila kujua Lyon amekuja kwa nidhamu ya kimchezo mwisho wa mechi mancity kajikuta kadondokea pua.

    Jibu

    Hongera sana lyon ila Man city walijiamini sana hii mechi bila kujua lyon wamekuja na kinizamu za michezo#Meridianbettz

    Jibu

    Hongera Lyon kwa kutufungia midomo ya man city

    Jibu

    Pongezi sana kwa Lyon mmeonyesha ushujaa wenu mbele ya man city

    Jibu

    Daaah kweli mpira na maajabu yakee aisee

    Jibu

    Safii Lyon kwatua mlio fikia inapendeza sana

    Jibu

    Hongera sana Lyon

    Jibu

    Me naona man city walisahau shauku yao kubwa walitaka kukutana na Bayern Munch sa walichokipata hiyo hinaitwa usitukane mamba kabla hauja vuka mto

    Jibu

    Pongezi kwa Lyon

    Jibu

    Keep it up Lyon

    Jibu

    Lyon wamejua kutuchania mkeka jamaniii

    Jibu

    Pongezi kwake

    Jibu

    pongezi kwao

    Jibu

    Unbelievable mwisho wa mashindano tusije tukashangaa kombe kabeba ambaye hatukumdhania.

    Jibu

    City waliingia kwa kujiamini sana ila kaunta atack walizotumia lyon ziliwanufaisha na kutoka kidedea

    Jibu

    Liyon ndio mabingwa msimu huu.

    Jibu

    Hngr zao

    Jibu

    Hongera sana Lyon ila hakuna aliyetegemea kama man city atatolewa na lyon

    Jibu

    Na hii ndo tuanita mpira dk 90

    Jibu

    Congrat Lyon Aibu kwa man city

    Jibu

    Mpira umetuonyesha maajabu yake

    Jibu

    Kinyume na matarajio yote, timu iliyomaliza katika nafasi ya saba katika msimu wa kandanda la Ufaransa, na ambayo ilikuwa imecheza mechi mbili pekee za ushindani tangu mapema Machi, sasa itacheza katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Jumatano dhidi ya Bayern Munich.

    Jibu

    Hiyo ndio the day of wonderfull football cz city walijiamin Sana walijua Lyon hawezi kupindua kumbe muda mwngn ht mtt anamzidi maarifa mkubwa.

    Jibu

    Hongera Sana Lyon

    Jibu

    Nilijua tu hili Gemu atashinda Lyon#Meridianbettz

    Jibu

    UEFA ya ajabu sana yani timu kubwakubwa zote zimetolewa ni jambo la kuhuzunisha maana watu tulijiwekea mazoea

    Jibu

    Hongera sana Lyon

    Jibu

    Wadau wengi tulikua tuna amini man u ndiye bingwa wa haya mashindano.

    Jibu

    hongera sana lyon

    Jibu

    Lyon walicheza mpira mzur sana tatizo la Manchester city walijiamin kupita kiasi

    Jibu

    Safi sana lyon

    Jibu

    hongera zao

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.