Klabu ya Manchester United imeanza kuandamwa na mzimu wa majeraha kwani jana katika mchezo wa kombe la Uefa Erupa League hatua ya robo fainali beki Lisandro Martinez na Raphael Varane walipata majeraha.
Manchester United imekua kwenye kiwango kizuri msimu huu wakiwa wamefanikiwa kubeba taji la Carabao, Lakini pia wapo nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi kuu ya Uingereza lakini ghafla klabu hiyo imeanza kuandamwa na majeraha mwishoni mwa msimu jambo ambalo linaonekana kua tishio.
Marcus Rashford, Alejandro Garnacho, Luke Shaw ni miongoni mwa wachezaji ambao walikua waliripotiwa kupata majeruhi wiki zilizopita, Lakini wachezaji wengine muhimu waliopata majeraha jana ni Raphael Varane na Lisandro Martinez ambao wamepata majeraha siku ya jana ni ndio mabeki tegemezi wakiwa kwenye kiwango bora kabisa.
Klabu ya Manchester United itawakosa wachezaji wake katika michezo kadhaa mbele na ni wachezaji muhimu ambao ni Lisandro Martinez, Varane, Garnacho na Luke Shaw lakini Marcus Rashford inaelezwa atakuepo katika mchezo unaofuata wa robo fainali dhidi ya Sevilla.
Klabu ya Manchester United imekua kwenye wakati mzuri sana kutokana na wachezaji wake muhimu kutokuandamwa na majeraha mara kwa mara hasa wale wanaoanza, Hivo kwasasa kinachosubiriwa ni kuangalia namna gani fomu ya klabu hiyo itakua baada ya kuandamwa na majeraha.

