Klabu ya Manchester United imeripotiwa kurejea kwenye mbio za kumuwania mshambuliaji wa klabu ya Tottenham Hotspurs na nahodha wa timu ya taifa ya Uingereza Harry Kane.
Manchester United wapo kwenye mchakato wa kutafuta mshambuliaji katika dirisha kubwa lijalo la majira ya joto, Klabu hiyo imekosa mshambuliaji halsi mwenye kiwango cha dunia kwa muda mrefu hivo Harry Kane amekua moja ya mchezaji anaefatiliwa kwa karibu zaidi.
Harry Kane ameshawahi kufatiliwa na klabu hiyo miaka kadhaa nyuma lakini haikunikiwa kumnasa nyota huyo, Lakini inaonekana kwasasa klabu hiyo imerudisha nguvu zake kwa staa huyo kutokana na kua na shida ya mshambuliaji wa katikati mwenye ubora wa kiwango cha dunia.
Manchester United inaelezwa wanatambua ugumu wa kumshawishi mwenyekiti wa klabu ya Tottenham Daniel Levy ambaye amekua mgumu kuuza wachezaji wake ndani ya ligi kuu ya Uingereza, Lakini watahakikisha wanafanikiwa kwenye jambo hilo msimu huu.
Klabu ya Man United tayari inazungmzwa kufanya mazungumzo na mshambuliaji Harry Kane na uongozi wake, Huku klabu hiyo ikiwa inaiombea dua mbaya klabu ya Tottenham isiweze kufuzu ligi ya mabingwa ulaya wakiamini itakua rahisi kumshawishi mchezaji huyo aweze kujiunga na mashetani wekundu hao.

