Matchday : Simba SC vs Dodoma JIJI FC

 

Klabu ya Simba SC itashuka dimbani kuvaana na klabu ya Dodoma Jiji katika mchezo wa ligi kuu ya NBC 2021/22 utakaopigwa katika uwanja wa Benjamin Mkapa majira ya saa moja kamili usiku.

 

Mchezo wa leo utakuwa wa pili wa mzunguko wa pili wa ligi kwa Simba SC baada ya ule wa kwanza dhidi ya Biashara United walioibuka na ushindi wa 3-0 siku ya Ijumaa.

Kocha wa Simba SC, Pablo Franco, ameweka wazi kuwa mchezo utakuwa mgumu na wataingia kwa tahadhari zote ili kukamilisha malengo ya kuchukua alama tatu muhimu.

“Ratiba ni ngumu, uwiano wa mechi moja na nyingine ni mdogo, hatuna muda wa kutosha kujiandaa na kufanya mazoezi ya utimamu wa mwili. Ndio maana tumekuwa na majeruhi wengi kikosini.

“Tunafahamu mchezo utakuwa mgumu, Dodoma ni timu nzuri lakini tumejipanga kuhakikisha tunawakabili na kuchukua pointi zote tatu,” aliongeza Pablo.


VUNA MKWANJA NA SHINDANO LA EVOPLAY SPRING AWEKING

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe