Tetesi za Soka Barani Ulaya.

Tetesi zinasema, Luis Suarez, 35 ataondoka Atletico Madrid msimu huu wa joto mkataba wake utakapomalizika. Mabingwa wa Italia, Inter Milan pamoja na Ajax, Sevilla na klabu kadhaa nchini Brazil zikiwania kumsajili mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uruguay.

Tetesi zinasema, Aston Villa wameambiwa kiungo wa kati wa Paris St-Germain Georginio Wijnaldum,31 atawagharimu pauni milioni 21.

 

Tetesi zinasema, Newcastle wako tayari kuweka mezani ofa ya £50m kumnunua winga wa Bayer Leverkusen Moussa Diaby, 22, huku klabu hiyo ya Ujerumani ikihitaji takriban £75m kumuachia.

Tetesi zinasema, Paris St-Germain wanataka kumsajili tena mshambuliaji wa Everton, Moise Kean, ambaye yuko Juventus kwa mkopo hadi msimu wa joto wa mwaka 2023.

Wakala wa Lautaro Martinez, Alejandro Camano anaonekana huenda amemaliza tetesi kuhusu Muargentina huyo kuhamia Arsenal, akisema kuwa mshambuliaji huyo wa miaka 24-atasalia San Siro.

Manchester United wamefikia makubaliano ya kumsajili kiungo wa kati Toby Collyer,18 baada ya mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Uingereza wa chini ya miaka-17 kushindwa kukubaliana mkataba mpya na Brighton.

 

West Ham wamepiga hatua kubwa katika juhudi za kumsaka mshambuliaji wa Udinese wa miaka 27-Mhispania Gerard Deulofeu, ambaye pia anasemekana huenda akarejea AC Milan.

Tetesi zinasema, Inter Milan wamewasiliana na wakala wa mshambuliaji wa Argentina Paulo Dybala, 28, ambaye mkataba wake na Juventus unamalizika mwisho wa msimu huu.


Vuna Mkwanja na Shindano la Evoplay Spring Aweking

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

Soma Zaidi Hapa

Acha ujumbe