Kocha wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola ameweka wazi kuwa klabu yake inahitaji mshambuliaji ili kuweza kupata mrithi wa kudumu wa kuziba pengo la mshambuliji aliyeacha rekodi ya ufungaji kwenye klabu hiyo Sergio Aguero.
Pep Guardiola amekuwa akicheza bila ya kuwa na mshambuliaji wa kueleweka kwenye nafasi ya ushambuliaji misimu yote tokea aondoke Sergio Aguero kwenye klabu hiyo, huku kwenye nafasi hiyo akiwatumia zaidi Jesus. Foden na Raheem.

Man City kwenye majira ya kiangazi walijaribu mara kadhaa kutaka kumsajiri mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane kutoka Tottenham Hotspur lakini hawakuweza kufanikiwa mpaka dirisha la usajiri kufungwa.
“Nadhani klabu inahitaji mshambuliaji, kabisa, ndio tunacheza vizuri sana pasipo mshambuliaji kwa sababu tunashinda, siku tusiposhinda utasema tunahitaji mshambuliaji.” Pep Guardiola alinukuliwa na BBC akisema kabla ya mchezo wa baadae dhidi ya Manchester United kwenye dimba la Etihad.
Man City wanaongoza kwenye msimamo kwa point tatu akifuatiwa na Liverpool huku majogoo wakiwa na idadi kubwa ya magoli ya kufunga ukilingnisha na City
Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.


