Granada Wamfuta Kazi Robert Moreno

Klabu ya Granada C.F  inayoshiriki ligi kuu nchini Hispania La Liga wamemfungashia virago kocha wao Robert Moreno baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Valencia kwa 3-1 siku ya jumapili jioni.

Maamuzi hayo yalitolewa muda mchache baada ya mpira kuisha ambapo walichapisha waraka wa kumshukuru Robert Moreno kwenye mtandao wa timu hiyo kwa kazi alijotelea kwenye klabu hiyo.

Granada

Robert Moreno ameicha klabu ya Granada kwenye hatari ya kushuka daraja, huku wakiwa wamepishana pointi tatu na Alaves ambaye anamfuatia ambaye yuko kwenye nafasi ya 18, tetesi za Moreno kufungashiwa virago zilianza kusambaa mapema sana msimu huu, lakini alifanikiwa kubadili matokeo na kufanikiwa kusalia kwenye timu hiyo.

Tangu mwaka huu mwanzoni mambo yalibadilika tena Moreno ameshindwa kuipa tena matokeo klabu ya Granada, hadi hizi wiki za karibuni uvumi wa kufukwa kazi kutokuwa siri tena.

Kapteni wa timu hiyo German Sanchez, alitoka na kuelezea kwamba wachezaji wote wapo pamoja na kocha wao baada ya kupoteza kwenye mchezo dhidi ya Valencia, “sote tupo pamoja na kocha, tunapopoteza, tunapoteza wote na timu yote kwa ujumla, nadhani kocha anafanya kazi nzuri.”

Wakati wachezaji wanamtazamo huo, nae mmiliki alikuwa na mtazamo tofauti na kuona vitu tofauti, baada ya kushinda michezo mitano msimu huu mpaka sasa na kupoteza michezo saba ya mwisho hakukuwa na maneno zaidi ya kumfungashia virago.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe