Matchday : Simba SC vs Biashara United.

 

Klabu ya Simba SC leo itakua uwanjani kuvaana na klabu ya Biashara United katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku.

 

Simba SC imekua nje ya nchi kwa takribani wiki mbili kwa ajili ya michuano ya Shririkisho barani Afrika na leo wanarejea kuwavaa Biashara katika mzunguko wa pili wa ligi ya NBC.

Kocha wa Simba SC, Pablo Franco, amesema mchezo utakuwa mgumu na wataingia kwa kuiheshimu Biashara kutokana na ubora wao lakini amejipanga kuhakikisha wanashinda.

“Mchezo utakuwa mgumu, Biashara ni timu nzuri, ina wachezaji wazuri mmoja mmoja. Tunahitaji kushinda ili kupunguza idadi ya pointi iliyopo dhidi ya wanaongoza. Tunacheza katika Uwanja wa nyumbani na tunategemea kupata ushindi,” amesema Pablo.

Katika mchezo huo viungo Mzamiru Yassin na Rally Bwalya wamerejea kikosini baada ya kumaliza masuala yao ya kifamilia yaliyokuwa yakiwakabili wakati Chris Mugalu, Kibu Denis, Hassan Dilunga, Jonas Mkude, Aishi Manula na Sadio Kanoute watakua nje kutokana na majeraha.


KASINO YA MTANDAONI: EMOTICOINS SABABU YA KUVUNA ZAIDI.

Haijawahi kuwa rahisi hivi kwenye safari yako ya kuvuna mkwanja, kasino maridhawa ya meridianbettz inakuletea mchezo wa Emoticoins unaokupa nafasi ya kufanya safari yako kuwa rahisi zaidi. Wakati ni wako nafasi ni yako na Emoticoins.

senegal, Senegal Mabingwa AFCON 2021., Meridianbet

CHEZA HAPA.

Acha ujumbe