Macho yote yalikuwa kwake na Kylian Mbappé alifunga bao lake la kwanza la Real Madrid katika mechi yake ya kwanza ya kimashindano kwa klabu hiyo, dhidi ya Atalanta kwenye UEFA Super Cup.

Real Madrid iliifunga Atalanta 2-0 mjini Warsaw jana usiku na kuwafanya Mbappé na Federico Valverde kupata majina yao kwenye ukurasa wa mabao.
Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.
Mbappé alicheza mechi yake ya kwanza katika mechi ya ushindani akiwa na Real Madrid na kufunga dakika ya 68, akiongozwa na pasi ya Jude Bellingham.

Ushindi wa Real Madrid unamaanisha kwamba Carlo Ancelotti amekuwa kocha pekee kushinda Super Cup mara tano.
Baada ya ushindi huo sasa Real watarejea nyumbani kwaajili ya kujiandaa na Laliga ambapo mechi ya kwanza watacheza ugenini dhidi ya Mallorca huku timu hiyo chini ya Ancelloti wakipewa nafasi kubwa ya kubeba taji hilo.


