Mshambuliaji wa PSG, Lionel Messi alikataa kushikana mkono na kocha wake Pochettino wakati timu hiyo ikiivaa Lyon baada ya kutolewa katika mchezo huo wa Ligue 1.

Messi hakufurahishwa na kitendo cha kutolewa dakika ya 76′ ya mchezo wakati wakiwa sare ya 1-1.
Pochettino ametetea uamuzi wake wa kumtoa messi mchezoni, huku akisema makocha wapo kwaajili ya kufanya maamuzi ya kipi ni bora kwaajili ya timu.
“Kila mtu anajua tuna wachezaji bora katika timu.
“Tuna utajiri wa kikosi cha wachezaji 35. Kisha inabidi ufanye uamuzi. Kwa wale 11 watakao anza. Baadae ufanye maamuzi wakati mchezo ukiendelea.
“Muda mwingine maamuzi haya yanalipa na muda mwingine hayalipi. Ndio maana tunasimama mbele ya benchi la ufundi na kufikiria nini cha kufanya. Na maauzi hayo inabidi uyafanye iwe yatalipa au hayatalipa. iwe unapenda au hupendi.” aliongeza Pochettino.

Mchezo huo ulimalizika kwa PSG kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 yakifungwa na Paqueta 66′ Neymar 66’p na Icardi 90+2′.
Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.


