Mshambuliaji wa Tottenham Lucas Moura amevutiwa sana na mchezaji mwenzake Gabriel Jesus kufuatia mwanzo wake mzuri wa maisha Arsenal akiwa ametokea Manchester City msimu huu.
Wabrazil hao wawili Moura na Jesus watamenyana katika mchezo wa Dabi wa Jumamosi wa Kaskazini mwa London, ambao una umuhimu zaidi kwani ushindi kwa vijana wa Antonio Conte wa Spurs utawafanya kuwavuka The Gunners na kukwea kileleni mwa Ligi ya Primia.
Ili kupata ushindi, Spurs watahitaji kumuweka pembeni Jesus, jambo ambalo linaweza kuwa mbali na kazi rahisi ikizingatiwa kuwa amefunga mabao manne na kutoa pasi tatu za mabao katika mechi saba za ligi tangu ajiunge naye akitokea Manchester City.
Wakati wawili hao watakuwa wapinzani Jumamosi, Moura amefurahishwa na jinsi mshambuliaji huyo Jesus anavyozidi kufanya vyema hadi sasa katika kikosi cha Mikel Arteta ambacho kinaonekana kuhitaji kucheza klabu bingwa barani Ulaya.
“Mtoto alianza kufunga na haachi. Kwanza kwa upande wa kibinafsi, kwa upande wa urafiki, nina furaha sana kwake. Ni mvulana anayestahili sana, ubora wa juu,” Moura aliiambia Stats Perform”.
Mchezaji huyo alisema Gabriel Jesus aliondoka klabu kubwa na kwenda Arsenal, na anafanya vizuri sana huko timu nzima inafanya vizuri sana. Arsenal imekuwa ikicheza vizuri sana bila shaka itakuwa mechi nzuri sana kwa mashabiki kutazama.