Napoli Yamkimbilia Ndoye Baada ya Kupigwa Chini na United Kuhusu Garnacho

Napoli inaripotiwa kuwa imeanza mazungumzo ya kumsajili winga wa Bologna, Dan Ndoye, huku Manchester United wakikataa ofa ya ufunguzi ya €40m kwa ajili ya Alejandro Garnacho.

Napoli Yamkimbilia Ndoye Baada ya Kupigwa Chini na United Kuhusu Garnacho

Winga wa Bologna, Ndoye, ameonekana kama chaguo kuu la Napoli kuchukua nafasi ya Khvicha Kvaratskhelia endapo Manchester United wataendelea kukataa kuuza winga huyo mwenye umri wa miaka 20, Garnacho.

Pia meridianbet inatoa michezo ya kasino ya mtandaoni kama vile, Aviator, poker, Roullette, sloti na mingine kibao. Ingia meridianbet na ucheze sasa.

Kwa mujibu wa Gazzetta, Red Devils wamekataa ofa ya ufunguzi ya €40m kwa mchezaji huyu kutoka Argentina.

Hii si ya kushangaza ikizingatiwa kuwa vyanzo vingi kutoka Italia vinadai kuwa bei inayohitajiwa na Red Devils ni €80m.

Napoli Yamkimbilia Ndoye Baada ya Kupigwa Chini na United Kuhusu Garnacho
 

Garnacho bado ni chaguo la kwanza kwa Antonio Conte, na mawakala wa mchezaji wako karibu kufikia makubaliano na Partenopei, lakini kama Manchester United watapunguza bei yao bado hakujawa na uthibitisho.

Ndoye hivi karibuni amejadili nia ya Liverpool kumtaka, lakini upinzani wa Manchester United kwa Garnacho umesababisha Napoli kuanzisha mazungumzo ya kumsajili mchezaji huyu wa kimataifa wa Uswisi.

Kwa mujibu wa Gazzetta, Partenopei wapo tayari kutoa €30m kwa mchezaji huyu mwenye umri wa miaka 24. Ofa hiyo haitakuwa ya kutosha kwa Bologna, lakini mazungumzo kati ya vilabu viwili vitaendelea leo.

Acha ujumbe