PSG Yapigwa Faini na UEFA.


Klabu ya soka ya Ufaransa, Paris Saint-Germain (PSG) wametozwa faini ya Sh3.7 milioni kwa hatia ya kutorejea uwanjani kwa wakati uliostahili baada ya mapumziko ya kipindi cha kwanza walipokuwa wakivaana na Atalanta kwenye robofainali ya Klabu Bingwa Ulaya (UEFA).

PSG waliibuka washindi wa mechi hiyo iliyochezewa jijini Lisbon, Ureno mnamo Agosti 12, 2020 na hivyo kujikatia tiketi ya kuvaana na RB Leipzig ya Ujerumani kwenye hatua ya nusu-fainali kwa mara ya kwanza baada ya miaka 25. Nusu-fainali hiyo itapigiwa jijini Lisbon mnamo Agosti 18, 2020.

PSG Yapigwa Faini na UEFA.

Leipzig waliwabandua Atletico Madrid ya Uhispania kwenye hatua ya nane-bora kwa mabao 2-1, hii ikiwa idadi sawa ya mabao ambayo PSG walifunga dhidi ya Atalanta ya Italia.

Kocha Thomas Tuchel wa PSG pia ameonywa vikali na Uefa kwa kutowajibika ipasavyo na kuchangia kukawia kuanzishwa kwa kipindi cha pili wakati wa mechi dhidi Atalanta. Mechi hiyo ilicheleweshwa kwa dakika saba.

Uefa inawaadhibu PSG siku moja baada ya kuwatoza Sevilla faini ya Sh1.2 milioni kwa kuchelewa kufika uwanjani wakati wa mechi ya robo fainali ya Europa League iliyowakutanisha na Wolves mnamo Agosti 11, 2020.

 

PSG Yapigwa Faini na UEFA.

Sevilla ambao ni mabingwa mara tano wa kipute cha Europa League, waliwapokeza Wolves kichapo cha 1-0 katika mechi hiyo iliyowakatia tiketi ya kupepetana na Manchester United kwenye nusu fainali itakayoandaliwa mjini Dusseldorf, Ujerumani mnamo Agosti 16, 2020.


Umekuwa mteja muaminifu wa meridianbet? Basi fahamu kuwa kuna zawadi kibao hadi 5% ya pesa yako inarejeshwa kwako. Kila wiki unaweza kurudishiwa mpaka Tsh 250,000.

Soma zaidi

43 Komentara

    Sheria ni msumeno lazima ifuatwe!!!

    Jibu

    Nimependa sana sheria za michezo kwa wezetu wako vizuri kama ingekuwa kwetu kwa kweli ingekuwa iko vizuri sana na wawekezaji wangeongezeka zaidi ila hili hamna

    Jibu

    Makosa yapo ila kuna mkosa mengine yaangaliwe bac jamani. ukiangalia na ali ya uchumi sas hivi imepolomoka sana

    Jibu

    Ni sawa, ili iwe fundisho kwa wengine

    Jibu

    Itakua fundisho kwao na kwa wengine

    Jibu

    Sheria ifuatwe mkondo wake

    Jibu

    Maoni:sawa kabisa katika jili wenzetu ulaya hawajali ukubwa wa timu wanaitaji nidhamu

    Jibu

    vizuri hii iwe fundisho kwao na kwa vilabu vyengine

    Jibu

    PSG inatakiwa wawe makini zaidi

    Jibu

    Vizuri ili iwe fundisho kwao na kwa vilabu vingine#Meridianbettz

    Jibu

    Naona UEFA Wamepata njia ya kuvuna mkwanja baada ya Corona kutikisa ulimwengu sasahivi ukizingua kidogo unapitiwa na Rungu la UEFA

    Jibu

    Taasisi yoyote lazima iwe na utaratibu unaotakiwa kufuatwa na kuheshimiwa na watu wote. Hongera UEFA kwa kuendelea kupiga rungu timu zote zinazokiuka utaratibu#meridianbettz

    Jibu

    Pole Sana PSG Ila wanatakiwa kujifunza kutokana na makosa

    Jibu

    Poleni sana psg lakini ndivyo ilivyo lazima tujifunze kutokana na makosa pia haitojirudia tena

    Jibu

    Safii sana hii itakuwa kama funzo kwa timu zingine ambaozo zitakazo Keuka sheria na taratibu zote ambazo zilizowekwa kwa kufuatwa na kila timu kwangu hii imekaa poa sanaa watoto mabishoo wengi sijui wanaenda na vioo na vitana

    Jibu

    Psg wamewaangusha mashabiki wao sana.

    Jibu

    Sheria zilizowekwa lazima zizingatiwe na vilabu vyote ulimwenguni.

    Jibu

    Hilo ni funzo kwa wengine makosa yasijirudie

    Jibu

    Hii fundisho kwa wengine

    Jibu

    Hi ni sawa ili club nyingine zipatae fundisho

    Jibu

    Sheria ifuate mkondo wake ili iwe fundisho kwa wengine

    Jibu

    Nifundisho kwa wengine

    Jibu

    Litakua fundisho kwa vilabu vyote kuto heshimu sheria na kanuni zilizowekwa.

    Jibu

    safi sana

    Jibu

    Wapate adhabu iwe fundisho pia kwa wengine

    Jibu

    Ni moja ya fundisho

    Jibu

    Duuh noma Sana.

    Jibu

    UEFA wamepamba moto timu ikitereza kidogo tu fain

    Jibu

    Ni vzur wajfunze siku nyngne

    Jibu

    Duh Haki itendeke hapo

    Jibu

    Nimependa sana sheria za michezo kwa wezetu wako vizuri kama ingekuwa kwetu kwa kweli ingekuwa iko vizuri sana na wawekezaji wangeongezeka zaidi ila hili hamna

    Jibu

    Sawa sheria ifuatwe watajifunza kwa Hilo.

    Jibu

    Lazima hatua za kisheria za mpira zifatwe

    Jibu

    Jamani Pesa yote hii!!!Imeniuma kama nimetoa mie#Meridianbettz

    Jibu

    fundisho kwa wengine ata hao psg siku nyingine watatii muda

    Jibu

    Sheria ifuate mkondo wake

    Jibu

    Ni mfano mzuri kwa timu zisizo zingatia sheria.

    Jibu

    Duuh! Wenzetu wanasheria kal sana maana ata sevilla walipewa faini walipochelewa kureport uwanjan bac n Jambo la kuigwa hata TFF wanatakiwa wajifunze kupitia wenzetu

    Jibu

    sheria ni msumeno lazima ifatwe

    Jibu

    Sheria razima izingatiwe

    Jibu

    Lazima Sheria zifatwe

    Jibu

    Mpira una sheria, wanatakiwa kuzifuata

    Jibu

    Duuuh atar Sana

    Jibu

Acha ujumbe