Setien Kuishtaki Barcelona.


Kocha wa zamani wa Barcelona, Quique Setien na waliokuwa wasaidizi wake watatu wamefichua mpango wa kushtaki kikosi cha hicho kwa kutotii masharti ya kandarasi zao baada ya kufukuzwa mnamo Agosti 2020.

Kwa mujibu wa Setien na wenzake, Barcelona iliwapa notisi ya kukamilisha kandarasi zao mnamo Septemba 16 licha ya miamba hao wa soka duniani kuwatimua Agosti 17.

Aidha, Setien alisema kwamba hakuna yeyote katika benchi lake la ufundi pale Camp Nou alikuwa amelipwa fidia yoyote na barua ambayo yeye na wenzake walipewa na Barcelona mnamo Septemba 16 haikutaja mpango wowote wa kulipwa kwao.

 

Setien Kuishtaki Barcelona.

“Barua kutoka kwa Barcelona inaashiria kwamba kikosi hicho hakina mpango wowote wa kutimiza masharti ya mikataba tuliyokuwa nayo tangu Januari 14, 2020,” akasema Setien.

Barcelona walimfuta kazi Setien siku tatu baada ya kikosi hicho kudhalilishwa kwa kichapo cha 8-2 kutoka kwa Bayern Munich ya Ujerumani kwenye robo-fainali za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) jijini Lisbon, Ureno.

Kutimuliwa kwake kulimpisha mkufunzi Ronald Koeman aliyewahi kuvalia jezi za Barcelona kati ya 1989 na 1995. Koeman aliajiriwa baada ya kushawishika na kuacha kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi.

Setien ambaye pia amewahi kuinoa Real Betis, aliajiriwa na Barcelona mnamo Januari 2020 na alikuwa amesimamia jumla ya mechi 25 za Barcelona hadi kutimuliwa kwake.

Chini ya Setien, 61, Barcelona walikamilisha kampeni zao za msimu huu bila taji lolote kwa mara ya kwanza tangu 2008. Barcelona walikamilisha msimu huu kwenye La Liga katika nafasi ya pili kwa alama tano nyuma ya mabingwa Real Madrid.

 

Setien Kuishtaki Barcelona.

Kichapo ambacho Barcelona walifungwa na Bayern kwenye UEFA kilikuwa cha nne katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ambayo iliwabandua kwenye robo-fainali za kipute hicho cha bara Ulaya.

Quique alimrithi kocha Ernesto Valverde uwanjani Camp Nou mwanzoni mwa 2020.

Baada ya kumtimua Setien, Barcelona walisema: “Haya ndiyo maamuzi ya kwanza kati ya mengi ambayo tunalenga kuchukua katika juhudi za kukisuka upya kikosi chetu.”

Barcelona pia walimtangaza Ramon Planes kuwa mkurugenzi mpya wa kiufundi kambini mwao. Planes alikuwa msaidizi wa Eric Abidal aliyetimuliwa na Barcelona akiwa mkurugenzi wa spoti.


SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

42 Komentara

    Kama Barcelona hawakuwalipa hela zao.bc walikosea ilibidi walipwe stahiki zao

    Jibu

    Haki yake setien kupata kile anachostahili kama wao klabu ndio waliovunja mkataba huo

    Jibu

    Wangelipana yote yasingekuwepo@meridianbettz

    Jibu

    mtu anabidi alipwe haki zake

    Jibu

    Wangemalizana tu.sio poa kufika huko wanakotaka kufikishana

    Jibu

    Satien na wenzake wanahaki ya kudai fidia mbali na kuiongoza timu vibaya lakini mikataba inatakiwa izingatiwe

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    Inabidi walipwe fidia

    Jibu

    Itakua si fair play kwa Kufany hivyo

    Jibu

    Endapo watashinda kesi watapiga mpunga mrefu

    Jibu

    Duuh atari iyo#Meridianbettz

    Jibu

    Barca mpeni chake kama hamna issue nae

    Jibu

    Sheria ifate mkondo wake

    Jibu

    Endapo watashinda kesi watapiga pesa ndefu

    Jibu

    Hapo sheria hifuate mkondo wake tu aki hitumike na kama ukijulikana ni kweli bac uwongozi utakua hupo mashakini

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Wakati Makocha wawili wa Yanga wanafikiria kuchukua hatua za kisheria kudai malipo yao kwa mara ya kwanza kwangu nasikia timu ya ulaya inashindwa kutimiza jukumu la kimkataba kwa waajiriwa wao wa zamani#meridianbettz

    Jibu

    Mkala nzuri

    Jibu

    inabidi walipwe fidia

    Jibu

    Duuh sio powa kabisa kupelekana huko

    Jibu

    alipwe haki zake jamani

    Jibu

    Asante kwa taarifa#meridianbettz

    Jibu

    Wanapaswa wasimamie kwenye haki yao

    Jibu

    Inabidi alipwe

    Jibu

    Wangemlipa tu haki yake

    Jibu

    Ujanja mwing walipe

    Jibu

    Nouma Sana hiyo

    Jibu

    Sheria ipo ivyo ukivunja mkataba inabidi wamlipe sasa mbona Barcelona wanaleta janja ya nyani!!

    Jibu

    Asante kwataarifa@meridianbet

    Jibu

    Makala mazur

    Jibu

    Sheria itafuata mkondo wake

    Jibu

    Jambo la aibu kubwa sana kwa club kubwa Kama Barcelona

    Jibu

    🔥

    Jibu

    Duh majAnga kwl

    Jibu

    Angelipwa tu wasifikie hatua mbaya

    Jibu

    Daah hatar

    Jibu

    Haki yake setien kupata kile anachostahili kama wao klabu ndio waliovunja mkataba huo

    Jibu

    usipotimiza mashart lazima ushtakiwe

    Jibu

    Sheria ifatwe

    Jibu

    Safi kudai haki yake

    Jibu

    Duuh

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.