Meneja mpya wa klabu ya Aston Villa na Lejendi wa Liverpool, Steven Gerrard amesema amekuwa akimfwatilia Mason Mount na ni shabiki mkubwa wa mchezaji huyo wa England na Chelsea.

Mount amekuwa nguzo kubwa kwa Chelsea katika kipindi cha miaka 3 iliyopita akifanikiwa kucheza mara 130 ndani ya timu hiyo na kuingoza klabu hiyo kutwaa Ligi ya Mabingwa mwezi May.
Mount, 23 atakuwepo katika kikosi kitakachoelekea Villa Park katika mchezo wa Ligi kuu siku ya Boxing Day, na Gerrerad yupo makini kutokana na hatari zinazoweza kusababishwa na mchezaji huyo.
“Nimemuona akiwa anakua, Ni mchezaji tunu kwa taifa. Ni shabiki mkubwa wa Mason.
“Anacheza akiwa na tabasamu usoni. Anatengeneza, anafunga na tayari ni mshindi wa Ligi ya mabingwa, sidhani kama anahitaji mtu kama mimi kumpongeza.
“Lakini ninachoweza kusema ni shabiki mkubwa. Natumaini hata onyesha ubora wake wikiendi.” aliongeza Gerrard.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


