Ten Hag Amuambia Maguire Kuiga Fomu Yake ya Uingereza Akiwa Utd

Kocha mkuu wa Manchester United Erik ten Hag amemtaka Harry Maguire kuiga kiwango chake cha Uingereza akiwa na United ili kupambana kurejea kwenye kikosi cha Mashetani Wekundu.

 

Ten Hag Amuambia Maguire Kuiga Fomu Yake ya Uingereza Akiwa Utd

Maguire alianza mechi tatu pekee za Ligi ya Primia kwa United msimu huu kabla ya kwenda Kombe la Dunia akiwa na Uingereza na kuonekana katika michezo yote mitano katika kufuzu kwa robo fainali.

Gareth Southgate amerudia kumuunga mkono beki huyo wa kati kwenye hatua ya Kimataifa, ingawa Raphael Varane na Lisandro Martinez wamekuwa washirika wa Ten Hag wanaopendelewa na United msimu huu.

Baada ya Uingereza kuondolewa na Ufaransa siku ya Jumamosi, Ten Hag anatumai Maguire anaweza kurejea Old Trafford kwa kujiamini kutokana na uchezaji wake wa kuvutia akiwa Qatar.

Ten Hag Amuambia Maguire Kuiga Fomu Yake ya Uingereza Akiwa Utd

Ten Haga maesema kuwa; “Ninaweza tu kumuunga mkono. Nimeulizwa mara nyingi kama anatosha kunichezea na ni wazi anatosha kucheza katika kiwango cha juu, na kisha ni juu yake kuonyesha ujasiri huo uwanjani na hakuonyesha hivyo katika mechi zote za United.”

Kocha huyo aliendelea kusema beki huyo anapocheza kwa kujiamini kama sasa, yeye ni mchezaji muhimu sana kwao na ndivyo kila myu anatarajia. Na hicho ndicho ambacho Maguire anatarajia kutoka kwake kutokana na kuwa na kiwango cha juu zaidi.

Jeraha la misuli ya paja lilimfanya Maguire kuwa nje kwa sehemu za kampeni za Ligi Kuu ya United, ingawa hata akiwa fiti Ten Hag bado amewatumia Martinez, Varane na Victor Lindelof juu ya mchezaji huyo wa miaka 29.

Ten Hag Amuambia Maguire Kuiga Fomu Yake ya Uingereza Akiwa Utd

Ten Hag alihakikisha hana matatizo na Maguire na anasisitiza uchezaji mzuri utapelekea kurejea kwenye kikosi chake cha kwanza akisema kuwa anapomchagua Varane sio tkitu dhidi ya Harry, bali wakati mwingine ni kwasababu mchezaji mmoja ni bora zaidi kuliko mwingine.

“Tuna wachezaji 16 hadi 18 kwenye kikosi na hicho ndicho unachokihitaji katika kiwango cha juu ukitaka kucheza kwa ajili ya kutwaa mataji, idadi ya michezo yote tunatakiwa kuifunga halafu inahusu wachezaji wanaounda timu bora, na timu hiyo tutaichagua. Haihusiani na kuwa mtu binafsi.”

Ten Hag Amuambia Maguire Kuiga Fomu Yake ya Uingereza Akiwa Utd

Acha ujumbe