Ten Hag Athibitisha United Kuwaongezea Mikataba Wachezaji Wake Muhimu

Kocha wa klabu ya Manchester United Erik Ten Hag amethibitisha kua wapo kwenye mazungumzo ya kuwaongezea mikataba wachezaji wake muhimu ambao mikataba yao ipo ukingoni.

Kocha huyo amezungumza mapema leo kua klabu hiyi imeanza rasmi mazungumzo na wachezaji wake muhimu ili kuwaongezea mikataba ya muda mrefu ili waendelee kusalia klabuni hapo, Kuna wachezaji kadhaa ambao mikataba yao inakaribia kumalizika na kocha huyo anawahitaji kwenye mradi wake wa kujenga timu hiyo.ten hagWachezaji ambao mikataba yao inaelekea ukingoni ni Marcus Rashford, Diogo Dalot, Luke Shaw, Fred na kocha Ten Hag ameweka wazi anataka kutengeneza timu ya muda mrefu na wachezaji hao wanatakiwa kua ndani ya timu hiyo hivo wanahitajika kuongezewa mikataba.

Siku za hivi karibuni klabu ya Manchester United kupitia kocha wake ilielezzwa wapo kwenye mkakati wa kuwaongezea wachezaji wake mikataba ambao mikataba yao inaelekea ukingoni na wachezaji waliotajwa sana ni Marcus Rashford pamoja na Diogo Dalot, Lakini kocha huyo leo amezungumza na kuweka bayana sio hao tu akiwaongeza Fred na Luke Shaw.ten hagManchester United chini ya Erik Ten Hag inataka kutengeneza timu bora na ya muda mrefu, Hivo viongozi hawana budi kusikiliza mahitaji ya mwalimu kwajili ya ustawi wa timu hiyo ambayo inataka kurejesha makali yake yaliyopotea kwa muda mrefu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.