Kocha wa klabu ya Manchester United Erik Ten Hag amefanikiwa kua kocha bora wa ligi kuu ya Uingereza mwezi Febuari baada ya kuiongoza timu hiyo kupata matokeo mazuri ndani ya mwezi huo.
Ten Hag amefanikiwa kubeba tuzo hiyo baada ya kuwashinda makocha wenzake kama Antonio Conte wa Tottenham Hotspurs, Marco Silva wa Fulham, Hiyo ni baada ya kufanikiwa kuiongoza klabu hiyo kwa kiwango kikubwa ndani ya mwezi Febuari.
Klabu ya Manchester United ndani ya mwezi Febuari imefanikiwa kucheza michezo minne na kufanikiwa kushinda michezo mitatu kati yake, Huku ikisuluhu mchezo mmoja na kujikusanyia jumla ya alama 10 katika michezo minne ni wazi kocha huyo Ten Hag amekua kwenye kiwango bora ndani ya timu hiyo.
Kocha huyo wa kimataifa wa Uholanzi amefanikiwa kushinda tuzo hiyo ikiwa ni mara yake ya pili msimu huu kutwaa tuzo hiyo akifanikiwa kutwaa tuzo hiyo mwezi Septemba mwaka jana, Hivo kuendelea kuonesha ubora wake baada ya kutoa tuzo hiyo mwezi huu.
Kocha Erik Ten Hag amekua na wakati mzuri tangu ajiunge na klabu ya Manchester United mapema mwezi Mei mwaka jana, Mpaka sasa akifanikiwa kuipa United taji la kwanza baada ya miaka saba vilevile wakiwa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania mataji mengine matatu yaliyobakia baada ya kubeba Carabao.

