Osaka Ajiondoa Kwenye Australian Open

Bingwa mara nne Naomi Osaka amejiondoa kwenye mashindano ya Australian Open 2023.

 

Osaka Ajiondoa Kwenye Australian Open

Mjapani huyo mwenye umri wa miaka 25 ni mshindi mara mbili wa Australian Open (2019 na 2021), lakini waandaji wa mashindano hayo wamethibitisha leo hii kuwa hataongeza idadi hiyo mnamo 2023.

Bado hakuna sababu iliyotajwa kwa uamuzi wa Osaka, ingawa hajacheza tangu ajitoe kwenye michuano ya Pan Pacific Open mjini Tokyo mwezi Septemba.

Osaka Ajiondoa Kwenye Australian Open

Osaka alivumilia msimu mgumu wa 2022 kwenye mashindano makubwa, akipoteza katika raundi ya kwanza kwenye French Open na US Open, huku akitolewa katika raundi ya tatu ya Australian Open mwaka jana na hakushiriki Wimbledon kutokana na jeraha la Achilles.

Kujiondoa kwa mchezaji huyo bora wa zamani wa Dunia kunafuatia ile ya mchezaji bora wa kiume Carlos Alcaraz na mshindi mara saba Venus Williams kutokana na jeraha. Bingwa anayetawala wa single za wanawake Ash Barty pia amestaafu kufuatia ushindi wake Januari mwaka jana.

Osaka Ajiondoa Kwenye Australian Open

Kwa sasa Naomi ameorodheshwa katika nafasi ya 42 duniani na nafasi yake itachukuliwa na Dayana Yastremska kwenye droo kuu.

Acha ujumbe