Tetesi za Soka Barani Ulaya.

 

Tetesi zinasema, Chelsea wanamtaka mlinzi wa Barcelona na Marekani Sergino Dest, 21.

Wakala wa mshambuliaji wa Brazil na Manchester City Gabriel Jesus ameeleza kwamba nyota huyo mwenye miaka 25 amefanyà mazungumzo na Arsenal kuhusu uwezekano wa kuhamia huko.

Mipango ya usajili Manchester United katika dirisha lijalo imeingia mchanga baada ya viungo watatu inaowataka kukataa kwenda Old Trafford.

 

Tottenham wanavutiwa na wachezaji watatu wa Everton, akiwemo mshambuliaji mbrazil Richarlison, 25, winga muingereza Anthony Gordon, 21, mlinzi mwenye miaka 24 muingereza Ben Godfrey.

Dimitar Berbatov ameionya Tottenham kuhusu winga wa Korea, Son Heung-min ambaye amekuwa na kiwango bora ndani ya miaka 3 mfululizo akiwa klabuni hapo.

Tetesi zinasema, Manchester United imefahamishwa itapaswa kulipa kitita cha £85.5m kama wanataka kumsajili mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 23, kutoka Napoli msimu huu.

 

Declan Rice

West Ham imempa kiungo wa England Declan Rice, ambaye anasakwa na klabu za Chelsea na Manchester United, mkataba wa miaka 8 atakaolipwa £200,000 kwa wiki ili asalie klabuni hapo.

Tetesi zinasema, Wolves itamsajili kiungo mchezeshaji wa Sporting Lisbon na Ureno Joao Palhinha, 26, kama kiungo wake wa Ureno Joao Moutinho, 35 ataondoka.


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe