Tetesi za usajiri: mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial atakuwa huru kuondoka Manchester United dirisha la Januari,Barcelona wanaonekana kuhitaji huduma yake.
Manchester United golikipa Dean Henderson anataka kuachiwa kwa mkopo katika dirisha la Januari, Chelsea wanajiandaa kuwapa mikataba mipya wachazaji wao ambao ni Mason Mount, N’Golo Kante, na Jorginho.

Chelsea wako tayari kutoa £86milion kwa mlinzi wa PSG Marquinhos kwenye majira ya kiangazi, Manchester City wanamfuatilia mshambuliaji wa Real Sociedad Mikel Oyarzabal.
Tetesi zinasema, Marco Asensio, anaweza kuondoka Real Madrid kama hatapa nafasi kikosi cha kwanza msimu huu chini ya kocha Carlo Ancelotti.

Arsenal wanamuachia golikipa wao Bernd Leno katika dirisha la majira ya kiangazi, baada ya kuwasili kwa golikipa Aaron Ramsdale.
Mshambuliaji Dusan Vlahovic anahusishwa na kuhamia Tottenham majira ya kiangazi, lakini yeye anahitaji kubaki Fiorentina.
Barcelona wanampango wa kuachana na Ronald koeman baada ya kutoanza msimu vizuri huku wakihusishwa na Roberto Martinez kuwa mbadala wake.
Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.


