Rais wa klabu ya Barcelona Joan Laporta alitoa ujumbe mwingine kwa njia ya video kwa mashabiki wa Barcelona, ambapo aliwaomba waendelee kuisapoti timu.
Sare ya 1-1 kwa Barcelona dhidi ya Granada siku ya Jumatatu usiku ilipelekea mashabiki wengi kumtaka Ronald Koeman kuiacha timu hiyo lakini Laporta amewataka mashabiki kuwa watulivu.
“Habari, mashabiki wa Barcelona nawaomba muendelee kuisapoti timu yetu,” Ujumbe wa video ulianza.
“Timu inawahitaji, na wanawashukuru, unajua tunapitia kipindi kigumu na hiki ndiyo kipindi mnachopaswa kusimama nasi.
“Wiki hii Barcelona inakwenda kwa mashabiki wa klabu ya Palos de la Frontera.
“Tukiwa Cadiz tunawahakikishia timu itajaribu kushinda.
“Kuweni na utulivu, tunajua nini kinatakiwa kifanyike na tutalitatua.
Ni wakati wa ushindi mkubwa ukiwa na kasino bomba ya Lock a Luck, meridianbet wanakupa sababu ya ushindi, funga bahati yako ya ushindi ukiwa na mabingwa.


