Mchezaji wa klabu ya Man Utd Wan-Bissaka amepigwa marufuku ya kuendesha gari kwa miezi sita na faini ya £30,000 kwa kosa la kuendesha gari kwa kasi mwezi Septemba 2020.
Mchezaji huyo mwenye miaka 24 anayeichezea klabu ya manchester united nafasi ya mlinzi wa kulia mapema mwaka huu alikubali kuendesha gari bila ya kuwa na leseni wala bima imayomruhusu kufanya hivyo wakati aliposimamishwa na polisi mwezi june 23 wakati akirudi kutoka kwenye mapumziko nje ya nchi.

Leo jumatatu hukumu ya Wan-Bissaka imetolewa na amekutwa na hatia baada ya kushindwa kutoa taarifa sahihi udereva [leseni] kwa uendeshaji gari kwa kasi katika maeneo ya Bradford na West Yorkshire mwezi septemba 2020.
Wan-Bissak ambaye anaishi na mkewe akiwa na mtoto wa mwaka mmoja, wamepigwa faini ya £30,000 kwa kuendesha gari pasipo kuwa na vibali na pia wamepigwa ya £1,500 kwa jumla kwa kushindwa kuwasilsha taarifa za kuendeshwa gari kwa kasi.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


