Kocha mkuu wa timu ya Barcelona Xavi Hernandez ameshangazwa na chama cha soka nchini humo La Liga kwa kutokualishwa kwa mchezo wao leo dhidi ya Mallorca,
Barcelona itawakaosa wachezaji wake karibia wachezaji tisa kutokana na Uviko-19 na majeruhi na wachezaji ambao watakosekana ni Clement Lenglet, Dani Alves, Jordi Alba, Alejandro Balde, Gavi, Ousmane Dembele, Ez Abde, Philippe Coutinho na Sergino Dest lakini chama cha soka nchini Hispania kimeamua mchezo huo uendelee.

“Tutawatumia wachezaji wa team B na tutakwenda kutafuta ushindi, lakini tuna wachezaji 17 ambao tunawakosa, nina wasiwasi. Nina shangaa kwa nini hawakuahirisha, haileti maana, tuko katika hali mbaya sana akili ya kawaida ungetumika.” Alisema Xavi
Sheria ya La Liga zinaelekeza kuwa mchezo hautahailishwa ikiwa kuna wachezaji watano wa kikosi cha kwanza na wachezaji 13 wanaweza kupatika akiwepo na golikipa mmoja basi mchezo utachezwa.
Xavi anakibarua kizito cha kuivusha Barcelona kutoka nafasi ya saba baada ya kuachwa pointi 17 na timu inayoongoza ligi kwenye msimamo wa La Liga.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

