Nyota wa Chelsea, Romelu Lukaku yupo tayari kurejea Serie A baada ya kuwepo kwa muda mfupi klabuni Chelsea.
Nyota huyu alikamilisha uhamisho kutoka klabu yake ya Serie A, ambayo aliwika sana ya Inter Milan msimu uliopota wa joto kwa dau la €113m.
Kuna ripoti kuwa huenda staa huyu anajilaumu kurejea Chelsea, akiamini hilo lilikuwa kosa na alianza kufanyia kazi mapema mpango wake wa kurejea Inter.
Taarifa zinaripoti kuwa klabu hizi mbili tayari zimeshakubaliana ada ya uhamisho wa mkopo ya €8 pamoja na €4 kwenye vipengele vya bonasi kwa mujibu wa huduma yake uwanjani.
Mwanasheria wa Lukaku Sebastien Ledure, amenukuliwa akisema Lukaku anahitaji muda mwingine wa kuwepo Inter Milan.

Bila shaka staa huyu anaweza kukubali kuwa alifanya maamuzi ya haraka sana kurudi Chelsea, kwa kuwa amelazimika kukubali punguzo la mshahara kwa asilimia 35 ili aweze kurejea kwa mkopo Inter.
ALIYA’S WISHES
Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.

