Bruno Awashukuru Mashabiki UTD

Mshambuliaji wa klabu ya Manchester United Bruno Fernandez amewashukuru mashabiki zao kwa kusafiri mpaka Leicester kwaajili ya kuwapa ushirikiano wa kushangilia.

Bruno Awashukuru Mashabiki UTD

Bruno kupitia ukurasa wake wa Twitter ameposti ujumbe uliosomeka hivi;

“Alama tatu nyingine tukiwa ugenini, shukrani nyingi na za pekee kwa mashabiki waliosafiri nasi mpaka Leicester wenye hali ya hewa nzuri, sasa ni muda wa kuimarika na kurejea tena siku ya Jumapili”

Bruno Awashukuru Mashabiki UTD

Man Utd walikuwa ugenini dhidi ya Leicester City ambapo walipata ushindi mgumu wa bao 1-0, goli lililofungwa na Jardon Sancho aliyepokea pasi mujarabu kutoka kwa Marcus Rashford mnamo dakika ya 23, bao lililodumu mpaka filimbi ya mwisho ya mwamuzi.

Bruno Awashukuru Mashabiki UTD

Ushindi huo unakuwa ni wa tatu mfululizo kwa Man utd baada ya kushinda dhidi ya Liverpool, wakashinda tena mbele ya Southampton na ule wa jana ukakamilisha rekodi ya ushindi kwenye mechi 3 mfululizo.

Mchezo unaofuata watakutana na Arsenal waliopo nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi ya Uingereza ambao hawajapoteza mechi hata moja.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.