Valencia CF imepata usajili wa mmoja wa wafungaji mabao wa kuvutia zaidi katika karne ya 21 Edinson Cavani.

Kuna furaha kubwa sana huko Mestalla wakati dirisha la uhamisho likifikia tamati, kwani Valencia CF wamepata usajili mkubwa kwa kumleta Edinson Cavani. Mshambuliaji huyo wa Uruguay amekuwa akifunga mabao kote Ulaya kwa muongo mmoja na nusu, lakini hajawahi kucheza LaLiga Santander.

Sasa, mashabiki wa soka wa Hispania wataweza kufurahia talanta hii ya ajabu, ambaye kocha wa Valencia CF Gennaro Gattuso anafurahi kufanya naye kazi.

Akimzungumzia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35, Gattuso alisema:
“Huyu si mchezaji wa kawaida. Amefunga mabao mengi katika maisha yake ya soka na amecheza katika timu kubwa. Ninaelewa kwa nini watu wanafurahi, kwa sababu yeye ni bingwa. Nimefurahiya pia, kwa sababu ya jinsi anavyocheza, mawazo yake na kila kitu ambacho tumeona kwenye taaluma yake.
Wasifu wake umekuwa wa kuvutia na Cavani amewakilisha vilabu vikubwa, lakini bado kuna mambo kadhaa ambayo hayajulikani sana kuhusu hadithi yake.”

